Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud afanyiwa upasuaji

Tom Mathinji, BBC and BBC
1 Min Read

Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud amefanyiwa upasuaji wa bega katika muungano wa Milki za Kiarabu (UAE), afisi ya rais inasema.

Rais Mohamud anapata nafuu kutokana na upasuaji huo “mdogo”,ofisi yake ilisema Alhamisi.

Aidha afisi hiyo haikutoa maelezo zaidi juu ya kile kilichotokea kwenye bega lake.

Rais alikaa Abu Dhabi kwa siku chache, ambapo pia alikutana na maafisa wakuu wa Imarati, Shirika la Habari la Kitaifa la Somalia (Sonna) linaripoti.

Baadaye alisafiri hadi Riyadh, Saudi Arabia, kuhudhuria mkutano wa kilele wa Saudi-Afrika.

Tangu kuchaguliwa tena mwaka jana, Bw Mohamud amesafiri katika mataifa kadhaa, yakiwemo mataifa ya Ghuba, kutafuta uungwaji mkono kwa mashambulizi ya serikali yake dhidi ya al-Shabab.

Website |  + posts
Share This Article